Je, Ninapaswa Kusoma Biblia Mara Ngapi?

Kutenga muda kwa ajili ya mambo ya kiroho kunaweza kukulemea katika ulimwengu wa leo unaoenda kasi.

Iwe ni mfanyabiashara kijana ukishughulikia kazi na malezi, mwanafunzi anayeshughulikia hali ya kukosa uhakika, au mtu anayetafuta maana zaidi, mara nyingi swali hutokea: Ni mara ngapi ninapaswa kusoma Biblia ili kukua katika imani kweli kweli?

Hii sio tu kuhusu ratiba. Inahusu lishe la roho, uwazi katika maamuzi ya maisha, na nguvu kwa ajili ya mapambano ya kila siku.

Kwa hivyo, hebu tuangalie kile Biblia inachosema kuhusu usomaji wa kila siku, kwa nini kiwango cha usomaji ni muhimu zaidi kuliko ratiba, na jinsi ya kutengeneza tabia endelevu na inayoridhisha katika usomaji wa Biblia.

Haya ndiyo tutakayoshughulikia:

Ikiwa unatamani kuanza safari yako ya usomaji wa Biblia au kuweka sawa utaratibu wako wa sasa, hebu tuangalie mwelekeo wa kibiblia na hamasisho lilioandaliwa kuwa msingi katika maisha yako.

Kwa nini usomaji endelevu wa Biblia ni muhimu

Watu wengi huchukulia usomaji wa Biblia kama wajibu wa kidini au orodha ya mambo. Lakini ukweli ni kwamba, kusoma Maandiko kila siku ni zaidi ya kupata kibali kutoka kwa Mungu. Bali ni kujenga mahusiano hai, halisi, yaliyojengwa katika msingi wa upendo kwake.

Kama vile mahusiano yoyote yenye maana, kuwa na wakati mzuri ni muhimu. Kwa kusoma Biblia kila siku, tunaweza kugundua kile ambacho Mungu anataka tujifunze, kuzifahamu njia Zake, na kumfuata Yesu kwa ukaribu zaidi kila siku.

Katika Biblia yote, tunaona jinsi watu waliotembea na Mungu walivyotumia muda katika neno Lake. Kutoka kwa Daudi kutafakari juu ya sheria mchana na usiku hadi Yesu akinukuu Maandiko wakati alipojaribiwa, tunajifunza kwamba tabia endelevu haichochewi na sheria. Ni nidhamu inayotoa uhai, kama ambavyo tungefanya kwa ajili ya kitu chochote tunachokijali au kukifanya kuwa kipaumbele. Na kutanguliza usomaji wa Maandiko hutusaidia kuunganisha kanuni zake zisizopitwa na wakati katika maisha yetu, ambazo zinaweza kututia nguvu hata wakati maisha yanapoharibika.

Sasa kwa kuwa tumeona kwa nini tabia endelevu ni muhimu, hebu tujifunze kile Maandiko yanachosema kuhusu usomaji wa maandiko wa kila siku.

Biblia inasema nini kuhusu ibada ya kila siku

Maandiko yenyewe yanahimiza usomaji wa kila siku.

Katika Kumbukumbu la Torati 17:19, wafalme waliagizwa kusoma kutoka katika Kitabu cha Sheria maisha yao yote ili kujifunza kuheshimu na kuelewa nguvu za

Mungu na kushika amri zake. Vivyo hivyo, Zaburi 1:2 humsifu yule anayependezwa na sheria ya Mungu na kuitafakari mchana na usiku.
(Kwa uwazi, hii haimaanishi kusoma au kukariri Maandiko kila mara, mchana kutwa, kutofanya jambo lingine lolote. Hii inazungumzia juu ya kuyaweka mbele ya akili yako kila wakati.)

Mungu alipanga kuwa neno lake liwe chanzo cha kila siku cha nguvu, hekima, na furaha.

Na tukiitazama Biblia kwa ujumla wake, Agano la Kale linaonyesha thamani ya mafundisho ya kila siku, huku Agano Jipya likitilia mkazo jambo hili kupitia mfano wa Yesu. Yesu alijua Maandiko kwa undani na akayatumia kufundisha, kusahihisha, na kufariji (Luka 4:4, 8, 12, 18-19).

Tunapotumia muda katika Biblia kila siku, hatusomi maneno tu. Tunakutana na Mungu kwa njia halisi na binafsi.

Kujua kile Biblia inachosema ni muhimu, lakini tunawezaje kugeuza ujuzi huo kuwa mazoea halisi?

Kuandaa ratiba halisi ya usomaji

“Ninapaswa kusoma Biblia mara ngapi?” Swali bora zaidi linaweza kuwa, “Ninawezaje kufanya usomaji wa Biblia kuwa sehemu ya maisha yangu?”

Kwa wengi, wazo la kusoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja linaonakana kuwa wazo la kuogopesha. Lakini hata hivyo, huo ni mpango ambao watu wengi wameugeuza kuwa mazoea ya muda mrefu.

Lakini tabia endelevu haihitaji masaa kwa siku. Hata dakika 10 hadi 15 kila siku katika Neno la Mungu zinaweza kubadilisha moyo na akili yako.

Anza na mpango unaoendana mtindo wako wa maisha. Unaweza kusoma sura chache kila siku, kuzingatia sehemu tofauti kama Zaburi na Mithali, au kwa kubadilishana kati ya Agano la Kale na Jipya.

Fikiria usomaji wa Biblia kwa kuzingatia msingi wa mada au mwongozo wa ibada wa kila siku wa Maandiko. Kiini ni kutenga muda mahususi, labda asubuhi au kabla ya kulala, na kuifanya kuwa miadi takatifu.

Kumbuka, swala sio una kasi kiasi gani bali kina. Kusoma polepole na kwa maombi mara nyingi kunaweza kuwa na matokeo zaidi kuliko kukimbilia kupitia vitabu kadhaa.

Pia kumbuka, hata hivyo, kwamba hata mipango iliyowekwa vizuri wakati mwingine huenda mrama. Nini basi?

Nini hutokea unapokosa siku (au zaidi)

Hebu tukabiliane na hili: maisha hubadilika.

Kati ya kazi, familia, na majukumu, inawezekana kuruka siku hata wiki. Lakini kukosa muda kwa ajili ya kusoma Biblia hakumaanishi kwamba Mungu atatupuuza. Anatualika turudi kwa neema. Badala ya kukata tamaa, endelea tu pale ulipoishia.

Epuka kuona usomaji wa Biblia kama maonyesho. Ni mazungumzo. Ikiwa haujazungumza na rafiki kwa muda mrefu, hamuachi kuwa marafiki. Vivyo hivyo na

Mungu. Anatamani uhusiano, sio tamaduni. Kilicho muhimu ni moyo, shauku yako ya kumjua, kuelewa mapenzi Yake, na kumkaribia kila siku.

Je, unajiuliza namna unavyoweza kufanya usomaji wako wa Biblia kuwa endelevu na wa kuvutia? Hapa kuna baadhi ya zana ambazo zinaweza kusaidia.

Nyenzo na mitindo inayoweza kukusaidia kuwa na usomaji unaovutia

A Bible and an iPhone with a Bible app.

Image by congerdesign from Pixabay

Shukrani kwa teknolojia, kujihusisha na Neno la Mungu ni rahisi zaidi kuliko hapo awali.

Hapa kuna njia chache unazoweza kuzitumia kufanya usomaji wako kuwa bora na wenye maana:

  • Programu tumishi za Biblia: Nyingi hutoa mipango ya usomaji ambayo inakusaidia kujifunza vitabu au mada mbalimbali.
  • Biblia za Sauti: Zinafaa kwa watu walio katika shughuli—sikiliza unaposafiri au kufanya mazoezi.
  • Mwongozo wa Ibada: Tafakari fupi zenye maandiko kila siku ili kuifanya Biblia kuwa muhimu kwa maisha ya kila siku.
  • Bibilia za kujifunzia: Hutoa maelezo na muktadha wa kihistoria ambao unakuza uelewa.
  • Kusoma pamoja na wengine: Kujiunga na kikundi cha kujifunza Biblia au kujadili Maandiko na rafiki hukusaidia kubaki ukiwajibika na kupata maarifa mapya.

Chochote kinachokufaa, kumbuka tu kwamba lengo ni kuwa na muda pamoja na Mungu.

Ili kumfuata Yesu kwa ukaribu zaidi, jaribu kusoma sehemu mbalimbali, kama vile Mithali kwa ajili ya hekima, Zaburi ili kupata faraja, na Injili ili kujua tabia ya Yesu kwa undani zaidi.

Kukumbatia maisha yaliyojikita kwenye Neno la Mungu

Kusoma Biblia kila siku ni zaidi ya kuweka alama kwenye kisanduku, bali kusitawisha uhusiano unaoleta uhai pamoja na Mungu.

Ikiwa unasoma aya chache au sura kadhaa, cha muhimu ni kwamba unatumia wakati mzuri na Mungu kupitia Neno Lake. Biblia si kitabu tu. Ni sauti hai ya

Mungu, tayari kukuongoza katika nyanja zote za maisha (2 Timotheo 2:15, 3:16).

Je, uko tayari kuchukua hatua yako inayofuata?

Chagua mpango wa usomaji wa Biblia leo na anza kwa dakika chache tu. Utashangaa jinsi Mungu anavyozungumza unapotenga muda wa kusikiliza.

Anza safari hii kwa makala hii, “Naweza Kusomaje Biblia Yangu Zaidi?”

Pia, pata makala zinazoleta matokeo bora kuhusu imani kwenye tovuti yetu, sehemu ya makala kuhusu Imani kwenye HFA.

Pin It on Pinterest

Share This